Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Kenya Gor Mahia ndio timu iliyokuwa bize sana katika dirisha la uhamisho wachezaji kwenye ligi kuu Kenya lililokamilika Novemba 6 mwaka huu ,huku ikiwasajili wanandinga 17 wapya na kuwaachilia wengine 15 kuondoka kusaka lishe bora.
Western Stima pia iliwasajili wachezaji wengi wakiwa 16 na kuwaruhusu wengine 20 kugura wakati wanajeshi Ulinzi Stars wakiwam miongoni mwa timu ambazo zilisajili wachezaji wachache mno wakiwa wane.
Katika uhamisho AFC Leopards iliwasajili wachezaji 13 wapya pamoja na kocha Tomas Truch huku ikiwaachilia wachezaji wanane,Bandari Fc ikiwasajili wachezaji watano pekee wengi wao kutoka timu ya mwambao Coast Stima Fc nao wane wakaondoka .
Bidco United ilisajili wachezaji 11na kuwaruhusu 9 kuondoka nao Kakamega Homeboyz wakasajili wanandinga 9 huku 7 wakiondoka,kisha Sofapa ikanasa wachezaji 9 nao 12 wakagura.
Ifuatayo ni orodha kamili ya usajili wachezaji katika ligi kuu ya FKF .
Msimu mpya wa ligi kuu unatazamiwa kuanza Novemba 20 mwaka huu na kukamilika Mei mwakani.