Nicholas Muyoti ameteuliwa kuwa kocha mpya wa kilabu cha Wazito Fc kinachoshiriki ligi kuu ya soka humu nchini.
Hadi uteuzi wake Muyoti amekuwa kocha wa Kakamega Homeboyz alikosajili matokeo mazuri huku akiwa na imani kuendeleza matokeo hayo katika timu ya Wazito Fc.
Katika majukumu yake ya ukufunzi Muyoti atasaidiwa na aliyekuwa kocha wa Muhoroni Youth Jeff Odongo huku kipa mstaafu Mathews Ottomax akiwa mkufunzi wa makipa .

Muyoti anachukua jukumu la kuwanoa Wazito Fc kutoka kwa Fred Ambani ambaye alitimuliwa Jumatatu pamoja na wasaidizi wake wote akiwemo msaidizi wake Salim Babu na mkufunzi wa makipa Elias Otieno.
Timu hiyo ya Wazito ambayo zamani ilikuwa ya chuo kikuu cha Nairobi imekuwa na hulka ya kuwapiga kalamu makocha na wachezaji mara kwa mara na halieweki chanzo cha kufurushwa kwa Ambani na wasaidizi wake.